DAWA ZA ASILI ZA DKT. IBOU (HERBAL) ZINAVYOCHAGIZA KUIMARISHA AFYA ZA JAMII

Muonekano wa dawa za asili za aina mbalimbali katika duka la Dkt. Ibou (HERBAL)

.................................

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

TIBA Asilia imekuwa nguzo kubwa katika ustawi wa afya za jamii na imekuwa ni kimbilio la watu wengi.

Jitihada kubwa za tafiti ambazo zimekuwa zikifanywa na waganga wa tiba za asili zimeongeza dawa za kutibu magonjwa ya aina mbalimbali hivyo kuchagiza uboreshaji wa afya za wananchi.

Dkt. Yusuph Ibou ni mmoja kati ya watafiti wa dawa za tiba asili hapa nchini ambaye amegundua dawa yenye mchanganyiko wa miti sabini inayofanya vizuri katika kutibu magonjwa ya aina tofautitofauti.

Akizungumza na waandishi wa habari Dkt. Ibou anasema kupitia tafiti za dawa za asili anazo zifanya zimekuwa na tija hivyo kuwa kimbilio la watu wenye changamoto mbalimbali za kiafya.

“Dawa za asili zimekuwa zikihitajika sana hivyo sisi waganga wa tiba za asili tunapaswa kujidhatiti kufanya tafiti na kuanzisha viwanda vya kuzalisha dawa zetu hizi za asili ambazo zinaendelea kukubalika kwa jamii kutokana na ubora wake,” alisema Ibou.

Alisema dawa hizo wanazozizalisha zimekuwa zikisaidia kuimarisha afya za wananchi hivyo kujenga taifa lenye maendeleo na kueleza kuwa bila ya kuwepo kwa afya bora hakuna maendeleo yoyote yatakayoweza kufanyika.

Dkt. Ibou alitaja baadhi ya magonjwa yanayotibiwa na dawa alizozifanyia utafiti kuwa ni malaria sugu ambayo yana pona kwa siku saba baada ya kuzitumia, Typhoid,  minyoo mikubwa na midogo, vidonda vya tumbo na magonjwa ya ngozi.

Alitaja magonjwa mengine kuwa ni ngiri, maumivu ya viungo, kipanda uso, bawasiri na mengine mengi.

Dkt. Ibou (HERBAL) ofisi yake ipo Barabara ya Nane Msikiti wa Warangi jijini Dodoma na kwa mawasiliano zaidi piga simu namba 0686851664, 0767851664 na 0718858664.

Dkt. Yusuph Ibou akionesha dawa zake alizozifanyia utafiti na kusajiliwa na Serikali.
Dkt. Yusuph Ibou akiwa ofisini kwake Barabara ya Nane karibu na Msikiti wa Warangi Jijini Dodoma.

Taarifa hii imeandaliwa na Dotto Mwaibale na Raphael Gwasa namba ya simu 0754362990.
 

Post a Comment

0 Comments