WAZIRI ULEGA: BANDARI YA UVUVI YA KILWA MKOANI LINDI INA FAIDA KUBWA.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega akizungumza na waandishi wa habari alipotembelea mji mdogo wa Masoko,Wilaya ya Kilwa kuona ujenzi wa Bandari ya Uvuvi leo Septemba 14,2023.

.................................................. 

Na Said Hamdsni  Lindi.

 

WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega amesema kujengwa kwa Bandari ya Uvuvi Wilaya ya Kilwa,mkoani Lindi,kutafungua fursa mpya ya ajira na kukuza pato la Taifa.

Ulega ameyaeleza hayo wakati anazungumza na waandishi wa vyombo mbalimbali  vya habari alipotembelea mji mdogo wa Masoko,Wilaya ya Kilwa kuona ujenzi wake.

Waziri amesema ujenzi wa Bandari hiyo utapokamilika utachochea  ukuwaji uchumi kwa wananchi wa maeneo husika na kukuza pato la Taifa.

Ametaja faida zingine zitazopatikana kupitia Bandari hiyo ni pamoja na watanzania 30,000 kupata ajira na teknolojia ya shughuli zitakazoendelea.

Amesema sekta ya uvuvi pekee imeajiri  idadi ya watanzania wasiopungua milioni tano,wakiwemo mmoja mmoja kulingana na mnyororo wa thamani ya sekta hiyo.

Waziri Ulega amesema kukamilika kwa ujenzi wake itakuwa inapokea na kuweka Nanga Meli kubwa kumi za urefu wa mita 30 na Boti 300 za wavuvi wadogo kwa wakati mmoja.

Amesema ujenzi utapokamilika Bandari itakuwa na eneo la kuchakata samaki wabichi wavuvi wadogo na soko kubwa la mazao yanayotokana na Bahari.

Waziri Ulega amesema lengo la Serikali ni kuinua mikoa yote inayozungukwa na Bahari ya Hindi, Pwani Lindi,Mtwara,Dar es salaam na Tanga.

Amesema uzinduzi wa ujenzi huo utafanywa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan Septemba 19 mwaka huu, mji mdogo wa Masoko Wilaya ya Kilwa.

Bandari ya uvuvi Kilwa inajengwa na kampuni ya HEC kutoka Jamhuri ya watu wa China kwa gharama ya Sh. Bilioni 262.0 na utachukua muda wa miezi 36 hadi kukamilika kwake.

Mwanzoni akimkaribisha Waziri Ulega kuzungumza na waandishi hao,Mkuu wa Wilaya ya Kilwa,Christopher Ngubiagai alisema Kabla ya nchi yetu haijapata Uhuru kutoka kwa utawala wa kikoloni Kilwa ilikuwa na maendeleo ya kiuchumi kwa kuwa na Salafu yake.

Ngubiagai alisema kuondoka utawala wa wakoloni akiwemo Ebuni Matuta miaka ya 1,331 Kilwa imedondoka kiuchumi kutokana na kukosekana viwanda na taasisi zinazochangia Ajira kwa wananchi.

Amesema kukamilika kwa Bandari hiyo kutaandika historia mpnz ya kiuchumi ndani ya Wilaya,Mkoa na Taifa.

Wakizungumzia ujenzi wa mradi wa Bandari hiyo Shaibu Juma,Selemani Serenge,Yusufu Saidi na Elena Mathias wanashukuru kupata mradi huo kwa madai utapungiza wimbi la umasikini kwa wananchi.


Post a Comment

0 Comments